Explore Swahili Poems (Mashairi)

Kuwa Nawe ni Ajali

by JackSwaleh

Yangu rununu hushiki, ujumbe sipati hata
Labda sijawafiki, usingehofu kusuta
Waona siwajibiki, kuelezwa sitakata
Hali sasa taharuki, mimi sitaki kujuta

Moyo wangu nilikupa, penzi lako nikazama
Nikakupenda kwa pupa, ukawa we...

Langu Waridi

by Kakakizzy

Uzuri wake waridi🌹, likupendeze machoni
Kwenye upepo baridi, harufu nzuri puani
Litimie ja ahadi, likaote mtimani
Mie mvua samaki, kwako nimevua lulu

Ipo Siku Naamini

by JackSwaleh

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali

Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Jumapili

by Kakakizzy

Mola Rabuka Manani, Mungu Mterehemezi
Leo twaja kwa imani, twazileta kwa Mwenyezi
Dua zetu za moyoni, Japo hatukupendezi
Ridhia kutujalia, yale tunayoombea

Kwenye Heri

by Kakakizzy

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Moyo Wangu Wasumbuka

by JackSwaleh

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu

Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Baba Wetu wa Mbinguni

by JackSwaleh

Baba wetu wa mbinguni, mbele zako nimerudi
Niko chini magotini, hali yangu inabidi
Kwa kukosoa imani, mema nikayakaidi
Nimepoteza ramani, pole kwa kubaidi

Yule mwovu kaninasa, kanipa vya ulimwengu
Kapiga zote anasa,...