Explore Swahili Poems (Mashairi)

Baba wetu wa mbinguni, mbele zako nimerudi
Niko chini magotini, hali yangu inabidi
Kwa kukosoa imani, mema nikayakaidi
Nimepoteza ramani, pole kwa kubaidi
Yule mwovu kaninasa, kanipa vya ulimwengu
Kapiga zote anasa,...

Amuka wenzangu, Sauti yaita
Yasije machungu, zuia utata
Umuombe Mungu, kwema kujikita
Na ndipo mkoko, waalika ua
Ninawausia, kesho si ahadi
Kifo chanukia, twafata wa jadi
Ndio yetu njia, hatuna zaidi
Na ndipo mkoko,...

Vuta nikuvute tena, mwenzanguwe kulikoni
Maneno mengi wachana, wewe huna hata soni
Yalibakia ya jana, sababuyo siioni
Huchoki kukimbizana, kwani kageuka jini
Usinitie kiwewe, wachana nami kabisa
Usitupe kwangu mawe, iwe ni...

Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni
Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...

Mpungufu binadamu, yeyote kiasi chake
Kuwa kamili adimu, kila mja na makeke
Yeyote yamugharimu, kuficha ubaya wake
Ni hujuma kulaumu, ati sema ikutoke
Kunena siwe mwepesi, legeza za kwako ndewe
Waelewe adinasi, usipo waache...

Sababu za sababu hizi nini
Sababu yako haswa ni nini
Lawama, ni nani wa kulaumu
Lawama na sababu zitaisha lini
Kama si sababu ni lawama
Basi ni sababu za lawama
Lawama za sababu hadi lini

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...