Explore Swahili Poems (Mashairi)

Nakukosea kwa kweli, nimekosa kutimiza
Ni ile ile tu hali, ya kesho yabaki giza
Sijui cha kubadili, nashinda nikikuwaza
Naanza kujikubali, kuwa nawe sitaweza
Ajira nimeshikika, bosi hatuelewani
Muda hata wa kupoka, naukosa...

Sababu za sababu hizi nini
Sababu yako haswa ni nini
Lawama, ni nani wa kulaumu
Lawama na sababu zitaisha lini
Kama si sababu ni lawama
Basi ni sababu za lawama
Lawama za sababu hadi lini

Nyimbo zangu barabara, kwa lugha ya Kiswahili
Viwango vya maabara, utunzi haujafeli
Mbinu yangu sijapora, jua akili ni mali
Kila siku nitachora, ubunifu hu ni ghali
Nipe kalamu mi bubu, nataka kusemezana
Makini na taratibu,...

Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake
Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni
Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

Nilipotoka ni mbali, kesho nayo majaliwa
Namshukuru Jalali, maisha kanipa mbawa
Kanilinda zote hali, kwangu tamu tu mliwa
Hapa ni kwangu manzili, mie nimebarikiwa
Raha ninayo moyoni, fikira nazo tulivu
Wa pili shajua nani,...

Mola Rabuka Manani, Mungu Mterehemezi
Leo twaja kwa imani, twazileta kwa Mwenyezi
Dua zetu za moyoni, Japo hatukupendezi
Ridhia kutujalia, yale tunayoombea