Explore Swahili Poems (Mashairi)

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu
Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Nyimbo zangu barabara, kwa lugha ya Kiswahili
Viwango vya maabara, utunzi haujafeli
Mbinu yangu sijapora, jua akili ni mali
Kila siku nitachora, ubunifu hu ni ghali
Nipe kalamu mi bubu, nataka kusemezana
Makini na taratibu,...

Mola Rabuka Manani, Mungu Mterehemezi
Leo twaja kwa imani, twazileta kwa Mwenyezi
Dua zetu za moyoni, Japo hatukupendezi
Ridhia kutujalia, yale tunayoombea

Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia
Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka

Zangu zifike salamu, nangoja yako jawabu
Bado niko mumu humu, kaniachia taabu
Najikaza nasaumu, rudi naomba jaribu
Niambie utakamu, gonjwa hili ulitibu
Hukunipa mi ilani, hata ya mwisho kwaheri
Ulienda pande gani, pekee...

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali
Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Ni nyingi kelele akilini
Napotulia, akili mna kelele
Nitalia hadi lini — ninazidiwa
Napojaribu kutulia, kengele zaongezeka
Ama natokwa na wazimu mimi
Naona ni kama sijielewi
Ni nyingi kelele akilini

Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni
Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...