Explore Swahili Poems (Mashairi)

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Angalau rudi baba, tusemezane kwaheri
Mchungu sana hu mwiba, hadi naumwa sadiri
Tumepatwa na msiba, ni nani katusihiri
Simanzi limetukaba, kifo kimekusairi
Sote tumekuwa bubu, sauti zimetutoka
Hii nayo ni sulubu, chozi...

Amuka wenzangu, Sauti yaita
Yasije machungu, zuia utata
Umuombe Mungu, kwema kujikita
Na ndipo mkoko, waalika ua
Ninawausia, kesho si ahadi
Kifo chanukia, twafata wa jadi
Ndio yetu njia, hatuna zaidi
Na ndipo mkoko,...

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali
Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Zangu zifike salamu, nangoja yako jawabu
Bado niko mumu humu, kaniachia taabu
Najikaza nasaumu, rudi naomba jaribu
Niambie utakamu, gonjwa hili ulitibu
Hukunipa mi ilani, hata ya mwisho kwaheri
Ulienda pande gani, pekee...

Nakukosea kwa kweli, nimekosa kutimiza
Ni ile ile tu hali, ya kesho yabaki giza
Sijui cha kubadili, nashinda nikikuwaza
Naanza kujikubali, kuwa nawe sitaweza
Ajira nimeshikika, bosi hatuelewani
Muda hata wa kupoka, naukosa...

Moyo wangu waugua, nasononeka kwa ndani
Nguvu zinanipungua, yaniishia imani
Laiti ningali jua, kiburi changu kiini
Nayo nishaichemua, mbelezo narudi chini
Tangu ulipoondoka, ni kweli kimeniramba
Mwenzio nahangaika, jinsi...

Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni
Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...

Baba wetu wa mbinguni, mbele zako nimerudi
Niko chini magotini, hali yangu inabidi
Kwa kukosoa imani, mema nikayakaidi
Nimepoteza ramani, pole kwa kubaidi
Yule mwovu kaninasa, kanipa vya ulimwengu
Kapiga zote anasa,...

Niwacheni tu jamani, hamuwezi nielewa
Zimezidi zenu shani, semi zenu zaniwawa
Mwang'ata kama kunguni, mwaumiza kama chawa
Haya yangu madhumuni, najua sijachelewa
Mzaha sasa usaha, mie munanihujumu
Raha sasa karaha, kamwe...

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Vuta nikuvute tena, mwenzanguwe kulikoni
Maneno mengi wachana, wewe huna hata soni
Yalibakia ya jana, sababuyo siioni
Huchoki kukimbizana, kwani kageuka jini
Usinitie kiwewe, wachana nami kabisa
Usitupe kwangu mawe, iwe ni...