Explore Swahili Poems (Mashairi)

Naamini Nitafika

by JackSwaleh

Nyimbo zangu barabara, kwa lugha ya Kiswahili
Viwango vya maabara, utunzi haujafeli
Mbinu yangu sijapora, jua akili ni mali
Kila siku nitachora, ubunifu hu ni ghali

Nipe kalamu mi bubu, nataka kusemezana
Makini na taratibu,...

Kwenye Heri

by Kakakizzy

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Usiku Bila Nuru

by JackSwaleh

Usiku bila nuru, kimya kote katanda
Kichwa mawazo nduru, hakuna lepe kitanda
Njia zote fungika, tayari fika mwisho
Gumu hili labaka, Mola nipangie kesho

Ngumu swali kujibu, kuelewa hali yangu
Sezi mimi bubu, kueleza soni...

Kwaheri ya Kuonana

by JackSwaleh

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu

Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Ndoa Ndoano

by Kakakizzy

Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake

Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...

Ipo Siku Naamini

by JackSwaleh

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali

Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Mawazo Waziwazi

by JackSwaleh

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza

Hayawi Hayawi Huwa

by JackSwaleh

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka

Natamani

by Kakakizzy

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni

Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

Niwacheni Tu Jamani

by JackSwaleh

Niwacheni tu jamani, hamuwezi nielewa
Zimezidi zenu shani, semi zenu zaniwawa
Mwang'ata kama kunguni, mwaumiza kama chawa
Haya yangu madhumuni, najua sijachelewa

Mzaha sasa usaha, mie munanihujumu
Raha sasa karaha, kamwe...

Tamu Imekuwa Chungu

by JackSwaleh

Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia

Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...

Lawamu Za Sababu

by JackSwaleh

Sababu za sababu hizi nini
Sababu yako haswa ni nini
Lawama, ni nani wa kulaumu
Lawama na sababu zitaisha lini
Kama si sababu ni lawama
Basi ni sababu za lawama
Lawama za sababu hadi lini