Explore Swahili Poems (Mashairi)

Nilipotoka ni Mbali

by JackSwaleh

Nilipotoka ni mbali, kesho nayo majaliwa
Namshukuru Jalali, maisha kanipa mbawa
Kanilinda zote hali, kwangu tamu tu mliwa
Hapa ni kwangu manzili, mie nimebarikiwa

Raha ninayo moyoni, fikira nazo tulivu
Wa pili shajua nani,...

Uanadamu Adimu

by JackSwaleh

Ni kweli wakati wote nakaa mwenye hasira
Ni kweli kabisa sura yangu imekunjika
Ukinitazama ni kama sina furaha yoyote
ni kama sina fani kwa lolote
Ni kweli nimesononeka
Ni kweli haya yote
Maisha yangu yote nimekuwa...

Angalau Rudi Baba

by JackSwaleh

Angalau rudi baba, tusemezane kwaheri
Mchungu sana hu mwiba, hadi naumwa sadiri
Tumepatwa na msiba, ni nani katusihiri
Simanzi limetukaba, kifo kimekusairi

Sote tumekuwa bubu, sauti zimetutoka
Hii nayo ni sulubu, chozi...

We mnyang'anyi jameni

by JackSwaleh

We mnyang'anyi jameni, sasa mbona hivi kweli
Nasema nawe mhuni, waona hii halali?
Nimechumia juani, usiku pia silali
Sasa hapo kivulini, wakula ya kwangu mali

Wazunguka na kiburi, kwangu chungu na machozi.
Mjini sasa ni...

Kwaheri ya Kuonana

by JackSwaleh

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu

Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Hayawi Hayawi Huwa

by JackSwaleh

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka

Kwenye Heri

by Kakakizzy

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Usiku Bila Nuru

by JackSwaleh

Usiku bila nuru, kimya kote katanda
Kichwa mawazo nduru, hakuna lepe kitanda
Njia zote fungika, tayari fika mwisho
Gumu hili labaka, Mola nipangie kesho

Ngumu swali kujibu, kuelewa hali yangu
Sezi mimi bubu, kueleza soni...

Zangu Zifike Salamu

by JackSwaleh

Zangu zifike salamu, nangoja yako jawabu
Bado niko mumu humu, kaniachia taabu
Najikaza nasaumu, rudi naomba jaribu
Niambie utakamu, gonjwa hili ulitibu

Hukunipa mi ilani, hata ya mwisho kwaheri
Ulienda pande gani, pekee...

Tamu Imekuwa Chungu

by JackSwaleh

Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia

Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...

Ipo Siku Naamini

by JackSwaleh

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali

Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Moyo Wangu Waugua

by JackSwaleh

Moyo wangu waugua, nasononeka kwa ndani
Nguvu zinanipungua, yaniishia imani
Laiti ningali jua, kiburi changu kiini
Nayo nishaichemua, mbelezo narudi chini

Tangu ulipoondoka, ni kweli kimeniramba
Mwenzio nahangaika, jinsi...