Explore Swahili Poems (Mashairi)

Zangu Zifike Salamu

by JackSwaleh

Zangu zifike salamu, nangoja yako jawabu
Bado niko mumu humu, kaniachia taabu
Najikaza nasaumu, rudi naomba jaribu
Niambie utakamu, gonjwa hili ulitibu

Hukunipa mi ilani, hata ya mwisho kwaheri
Ulienda pande gani, pekee...

Hali Gani Hii Ghali

by JackSwaleh

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu

Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Tamu Imekuwa Chungu

by JackSwaleh

Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia

Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...

Uanadamu Adimu

by JackSwaleh

Ni kweli wakati wote nakaa mwenye hasira
Ni kweli kabisa sura yangu imekunjika
Ukinitazama ni kama sina furaha yoyote
ni kama sina fani kwa lolote
Ni kweli nimesononeka
Ni kweli haya yote
Maisha yangu yote nimekuwa...

Mpungufu Binadamu

by JackSwaleh

Mpungufu binadamu, yeyote kiasi chake
Kuwa kamili adimu, kila mja na makeke
Yeyote yamugharimu, kuficha ubaya wake
Ni hujuma kulaumu, ati sema ikutoke

Kunena siwe mwepesi, legeza za kwako ndewe
Waelewe adinasi, usipo waache...

Angalau Rudi Baba

by JackSwaleh

Angalau rudi baba, tusemezane kwaheri
Mchungu sana hu mwiba, hadi naumwa sadiri
Tumepatwa na msiba, ni nani katusihiri
Simanzi limetukaba, kifo kimekusairi

Sote tumekuwa bubu, sauti zimetutoka
Hii nayo ni sulubu, chozi...

Vuta Nikuvute Tena

by JackSwaleh

Vuta nikuvute tena, mwenzanguwe kulikoni
Maneno mengi wachana, wewe huna hata soni
Yalibakia ya jana, sababuyo siioni
Huchoki kukimbizana, kwani kageuka jini

Usinitie kiwewe, wachana nami kabisa
Usitupe kwangu mawe, iwe ni...

Penzi Kibarua

by JackSwaleh

Nakukosea kwa kweli, nimekosa kutimiza
Ni ile ile tu hali, ya kesho yabaki giza
Sijui cha kubadili, nashinda nikikuwaza
Naanza kujikubali, kuwa nawe sitaweza

Ajira nimeshikika, bosi hatuelewani
Muda hata wa kupoka, naukosa...

Lawamu Za Sababu

by JackSwaleh

Sababu za sababu hizi nini
Sababu yako haswa ni nini
Lawama, ni nani wa kulaumu
Lawama na sababu zitaisha lini
Kama si sababu ni lawama
Basi ni sababu za lawama
Lawama za sababu hadi lini

We mnyang'anyi jameni

by JackSwaleh

We mnyang'anyi jameni, sasa mbona hivi kweli
Nasema nawe mhuni, waona hii halali?
Nimechumia juani, usiku pia silali
Sasa hapo kivulini, wakula ya kwangu mali

Wazunguka na kiburi, kwangu chungu na machozi.
Mjini sasa ni...

Kwaheri ya Kuonana

by JackSwaleh

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu

Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Mkoko Waalika Ua

by Kakakizzy

Amuka wenzangu, Sauti yaita
Yasije machungu, zuia utata
Umuombe Mungu, kwema kujikita
Na ndipo mkoko, waalika ua

Ninawausia, kesho si ahadi
Kifo chanukia, twafata wa jadi
Ndio yetu njia, hatuna zaidi
Na ndipo mkoko,...