Explore Swahili Poems (Mashairi)

Mpungufu Binadamu

by JackSwaleh

Mpungufu binadamu, yeyote kiasi chake
Kuwa kamili adimu, kila mja na makeke
Yeyote yamugharimu, kuficha ubaya wake
Ni hujuma kulaumu, ati sema ikutoke

Kunena siwe mwepesi, legeza za kwako ndewe
Waelewe adinasi, usipo waache...

Hali Gani Hii Ghali

by JackSwaleh

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu

Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Moyo Wangu Waugua

by JackSwaleh

Moyo wangu waugua, nasononeka kwa ndani
Nguvu zinanipungua, yaniishia imani
Laiti ningali jua, kiburi changu kiini
Nayo nishaichemua, mbelezo narudi chini

Tangu ulipoondoka, ni kweli kimeniramba
Mwenzio nahangaika, jinsi...

Ipo Siku Naamini

by JackSwaleh

Ipo siku naamini, ya kwangu yatabadili
Yatanitoka moyoni, iwe bora tena hali
Utulivu akilini, isizame yangu meli
Nikapate tu amani, dua langu kwa Jalali

Ipo siku ndugu yangu, utatabasamu tena
Yataisha tu machungu, shida...

Zangu Zifike Salamu

by JackSwaleh

Zangu zifike salamu, nangoja yako jawabu
Bado niko mumu humu, kaniachia taabu
Najikaza nasaumu, rudi naomba jaribu
Niambie utakamu, gonjwa hili ulitibu

Hukunipa mi ilani, hata ya mwisho kwaheri
Ulienda pande gani, pekee...

Niwacheni Tu Jamani

by JackSwaleh

Niwacheni tu jamani, hamuwezi nielewa
Zimezidi zenu shani, semi zenu zaniwawa
Mwang'ata kama kunguni, mwaumiza kama chawa
Haya yangu madhumuni, najua sijachelewa

Mzaha sasa usaha, mie munanihujumu
Raha sasa karaha, kamwe...

Langu Waridi

by Kakakizzy

Uzuri wake waridi🌹, likupendeze machoni
Kwenye upepo baridi, harufu nzuri puani
Litimie ja ahadi, likaote mtimani
Mie mvua samaki, kwako nimevua lulu

Kwaheri ya Kuonana

by JackSwaleh

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu

Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Natamani

by Kakakizzy

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni

Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

We mnyang'anyi jameni

by JackSwaleh

We mnyang'anyi jameni, sasa mbona hivi kweli
Nasema nawe mhuni, waona hii halali?
Nimechumia juani, usiku pia silali
Sasa hapo kivulini, wakula ya kwangu mali

Wazunguka na kiburi, kwangu chungu na machozi.
Mjini sasa ni...

Kwenye Heri

by Kakakizzy

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Mawazo Waziwazi

by JackSwaleh

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza