Explore Swahili Poems (Mashairi)

Moyo Wangu Waugua

by JackSwaleh

Moyo wangu waugua, nasononeka kwa ndani
Nguvu zinanipungua, yaniishia imani
Laiti ningali jua, kiburi changu kiini
Nayo nishaichemua, mbelezo narudi chini

Tangu ulipoondoka, ni kweli kimeniramba
Mwenzio nahangaika, jinsi...

Mawazo Waziwazi

by JackSwaleh

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza

Hayawi Hayawi Huwa

by JackSwaleh

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka

Niwacheni Tu Jamani

by JackSwaleh

Niwacheni tu jamani, hamuwezi nielewa
Zimezidi zenu shani, semi zenu zaniwawa
Mwang'ata kama kunguni, mwaumiza kama chawa
Haya yangu madhumuni, najua sijachelewa

Mzaha sasa usaha, mie munanihujumu
Raha sasa karaha, kamwe...

Tamu Imekuwa Chungu

by JackSwaleh

Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia

Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...

Kuwa Nawe ni Ajali

by JackSwaleh

Yangu rununu hushiki, ujumbe sipati hata
Labda sijawafiki, usingehofu kusuta
Waona siwajibiki, kuelezwa sitakata
Hali sasa taharuki, mimi sitaki kujuta

Moyo wangu nilikupa, penzi lako nikazama
Nikakupenda kwa pupa, ukawa we...

Mkoko Waalika Ua

by Kakakizzy

Amuka wenzangu, Sauti yaita
Yasije machungu, zuia utata
Umuombe Mungu, kwema kujikita
Na ndipo mkoko, waalika ua

Ninawausia, kesho si ahadi
Kifo chanukia, twafata wa jadi
Ndio yetu njia, hatuna zaidi
Na ndipo mkoko,...

Subira Yaniumiza

by JackSwaleh

Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni

Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...

Mpungufu Binadamu

by JackSwaleh

Mpungufu binadamu, yeyote kiasi chake
Kuwa kamili adimu, kila mja na makeke
Yeyote yamugharimu, kuficha ubaya wake
Ni hujuma kulaumu, ati sema ikutoke

Kunena siwe mwepesi, legeza za kwako ndewe
Waelewe adinasi, usipo waache...

Kelele Kengele

by JackSwaleh

Ni nyingi kelele akilini
Napotulia, akili mna kelele
Nitalia hadi lini — ninazidiwa
Napojaribu kutulia, kengele zaongezeka
Ama natokwa na wazimu mimi
Naona ni kama sijielewi
Ni nyingi kelele akilini

Kwaheri ya Kuonana

by JackSwaleh

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu

Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Uanadamu Adimu

by JackSwaleh

Ni kweli wakati wote nakaa mwenye hasira
Ni kweli kabisa sura yangu imekunjika
Ukinitazama ni kama sina furaha yoyote
ni kama sina fani kwa lolote
Ni kweli nimesononeka
Ni kweli haya yote
Maisha yangu yote nimekuwa...