This is Kakakizzy

author image

Kaka Kizzy!

My recent content

Hope

by Kakakizzy

Who will sing the song
That woke us up every morning
The blue bird chirps a melody
Sweet as it seems, we hear an elegy
The sun rises in the East
But it's not a new dawn
Just another day to be withdrawn
Whoever finds the...

Jumapili

by Kakakizzy

Mola Rabuka Manani, Mungu Mterehemezi
Leo twaja kwa imani, twazileta kwa Mwenyezi
Dua zetu za moyoni, Japo hatukupendezi
Ridhia kutujalia, yale tunayoombea

Kwenye Heri

by Kakakizzy

Kila siku ninasali, kusudi nikufikie
Mbinguni kulo muhali, nami nikashuhudie
Yaliyo semwa awali, sitaki nikajutie
Eti kunako asali, maziwa ni teletele

Langu Waridi

by Kakakizzy

Uzuri wake waridi🌹, likupendeze machoni
Kwenye upepo baridi, harufu nzuri puani
Litimie ja ahadi, likaote mtimani
Mie mvua samaki, kwako nimevua lulu

Mkoko Waalika Ua

by Kakakizzy

Amuka wenzangu, Sauti yaita
Yasije machungu, zuia utata
Umuombe Mungu, kwema kujikita
Na ndipo mkoko, waalika ua

Ninawausia, kesho si ahadi
Kifo chanukia, twafata wa jadi
Ndio yetu njia, hatuna zaidi
Na ndipo mkoko,...

Natamani

by Kakakizzy

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni

Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

Ndoa Ndoano

by Kakakizzy

Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake

Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...