Explore Swahili Poems (Mashairi)

Subira Yaniumiza

by JackSwaleh

Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni

Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...

Hayawi Hayawi Huwa

by JackSwaleh

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka

Nilipotoka ni Mbali

by JackSwaleh

Nilipotoka ni mbali, kesho nayo majaliwa
Namshukuru Jalali, maisha kanipa mbawa
Kanilinda zote hali, kwangu tamu tu mliwa
Hapa ni kwangu manzili, mie nimebarikiwa

Raha ninayo moyoni, fikira nazo tulivu
Wa pili shajua nani,...

Natamani

by Kakakizzy

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni

Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

Niwacheni Tu Jamani

by JackSwaleh

Niwacheni tu jamani, hamuwezi nielewa
Zimezidi zenu shani, semi zenu zaniwawa
Mwang'ata kama kunguni, mwaumiza kama chawa
Haya yangu madhumuni, najua sijachelewa

Mzaha sasa usaha, mie munanihujumu
Raha sasa karaha, kamwe...

Moyo Wangu Waugua

by JackSwaleh

Moyo wangu waugua, nasononeka kwa ndani
Nguvu zinanipungua, yaniishia imani
Laiti ningali jua, kiburi changu kiini
Nayo nishaichemua, mbelezo narudi chini

Tangu ulipoondoka, ni kweli kimeniramba
Mwenzio nahangaika, jinsi...

Usiku Bila Nuru

by JackSwaleh

Usiku bila nuru, kimya kote katanda
Kichwa mawazo nduru, hakuna lepe kitanda
Njia zote fungika, tayari fika mwisho
Gumu hili labaka, Mola nipangie kesho

Ngumu swali kujibu, kuelewa hali yangu
Sezi mimi bubu, kueleza soni...

Kelele Kengele

by JackSwaleh

Ni nyingi kelele akilini
Napotulia, akili mna kelele
Nitalia hadi lini — ninazidiwa
Napojaribu kutulia, kengele zaongezeka
Ama natokwa na wazimu mimi
Naona ni kama sijielewi
Ni nyingi kelele akilini

Ndoa Ndoano

by Kakakizzy

Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake

Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...

Naamini Nitafika

by JackSwaleh

Nyimbo zangu barabara, kwa lugha ya Kiswahili
Viwango vya maabara, utunzi haujafeli
Mbinu yangu sijapora, jua akili ni mali
Kila siku nitachora, ubunifu hu ni ghali

Nipe kalamu mi bubu, nataka kusemezana
Makini na taratibu,...

Mawazo Waziwazi

by JackSwaleh

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza

Mjini Kimeumana

by JackSwaleh

Mjini kimeumana, nazidiwa maarifa
Mazito yananibana, zinaongezeka nyufa
Najaribu kukazana, marefu sana masafa
Ndoto zabakia dhana, mkweche nango ja mafa

Maisha huku magumu, heri kule kijijini
Najificha mumu humu, nazidiwa na...