Explore Swahili Poems (Mashairi)

Siku nyingi natamani, udurusu ya moyoni
Hino zito ya uzani, niitoe mtimani
Ujuwe sina utani, ninapokuita hani
Siku niloitamani, leo dhahiri machoni
Jamani ninatamani, moyo ngekua kitabu
Ungefungua zamani, ewe waangu...

Mpungufu binadamu, yeyote kiasi chake
Kuwa kamili adimu, kila mja na makeke
Yeyote yamugharimu, kuficha ubaya wake
Ni hujuma kulaumu, ati sema ikutoke
Kunena siwe mwepesi, legeza za kwako ndewe
Waelewe adinasi, usipo waache...

Ni kweli wakati wote nakaa mwenye hasira
Ni kweli kabisa sura yangu imekunjika
Ukinitazama ni kama sina furaha yoyote
ni kama sina fani kwa lolote
Ni kweli nimesononeka
Ni kweli haya yote
Maisha yangu yote nimekuwa...

Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake
Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...

We mnyang'anyi jameni, sasa mbona hivi kweli
Nasema nawe mhuni, waona hii halali?
Nimechumia juani, usiku pia silali
Sasa hapo kivulini, wakula ya kwangu mali
Wazunguka na kiburi, kwangu chungu na machozi.
Mjini sasa ni...

Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...

Yangu rununu hushiki, ujumbe sipati hata
Labda sijawafiki, usingehofu kusuta
Waona siwajibiki, kuelezwa sitakata
Hali sasa taharuki, mimi sitaki kujuta
Moyo wangu nilikupa, penzi lako nikazama
Nikakupenda kwa pupa, ukawa we...

Ni nyingi kelele akilini
Napotulia, akili mna kelele
Nitalia hadi lini — ninazidiwa
Napojaribu kutulia, kengele zaongezeka
Ama natokwa na wazimu mimi
Naona ni kama sijielewi
Ni nyingi kelele akilini

Najawa na wasiwasi, sina kamwe utulivu
Moyo wapiga kwa kasi, zapungua zangu nguvu
Navunjika kwa wepesi, nakubali mi potovu
Taabu zinenikisi, nakaribia majivu
Mbona mie nasulubu, na jihisi takataka
Kuishi sina sababu, msukumo...

Ninayowaza siwezi eleza
Kueleza natatizika
Natatizika na haya mawazo
Mawazo kuyawazua yawe wazi
Nayawazia tena sana
Ninayowaza siwezi eleza

Usiku bila nuru, kimya kote katanda
Kichwa mawazo nduru, hakuna lepe kitanda
Njia zote fungika, tayari fika mwisho
Gumu hili labaka, Mola nipangie kesho
Ngumu swali kujibu, kuelewa hali yangu
Sezi mimi bubu, kueleza soni...

Hayawi hayawi huwa
Ukiona vyaelea jua vimeundwa
Kama halipo basi laja
Linalokusudi lina kusudi
Chunga usiwe mpango au mpangoni
Unayoyaona ni hivyo tu
Ajuaye pekee Maulana
Binadamu hugeuka