Explore Swahili Poems (Mashairi)
Tamu imekuwa chungu, raha geuka karaha
Nalilia nchi yangu, yadhorora yake siha
Kenya kipenzi chungu, nafata gani nasaha
Lavunjika hili jungu, tunaipoteza njia
Kosa gani tunatenda, vijana kujieleza
Raisi tunakupenda, sauti...
Angalau rudi baba, tusemezane kwaheri
Mchungu sana hu mwiba, hadi naumwa sadiri
Tumepatwa na msiba, ni nani katusihiri
Simanzi limetukaba, kifo kimekusairi
Sote tumekuwa bubu, sauti zimetutoka
Hii nayo ni sulubu, chozi...
Usiku bila nuru, kimya kote katanda
Kichwa mawazo nduru, hakuna lepe kitanda
Njia zote fungika, tayari fika mwisho
Gumu hili labaka, Mola nipangie kesho
Ngumu swali kujibu, kuelewa hali yangu
Sezi mimi bubu, kueleza soni...
Baba wetu wa mbinguni, mbele zako nimerudi
Niko chini magotini, hali yangu inabidi
Kwa kukosoa imani, mema nikayakaidi
Nimepoteza ramani, pole kwa kubaidi
Yule mwovu kaninasa, kanipa vya ulimwengu
Kapiga zote anasa,...
Nyimbo zangu barabara, kwa lugha ya Kiswahili
Viwango vya maabara, utunzi haujafeli
Mbinu yangu sijapora, jua akili ni mali
Kila siku nitachora, ubunifu hu ni ghali
Nipe kalamu mi bubu, nataka kusemezana
Makini na taratibu,...
Mjini kimeumana, nazidiwa maarifa
Mazito yananibana, zinaongezeka nyufa
Najaribu kukazana, marefu sana masafa
Ndoto zabakia dhana, mkweche nango ja mafa
Maisha huku magumu, heri kule kijijini
Najificha mumu humu, nazidiwa na...
Subira yaniumiza, yatakuwa sawa lini
Hali kweli imekaza, nachotaka sikioni
Jasho bure kupanguza, nasubiriyo laini
Nguvuzo nitajijaza, kujikaza kisabuni
Maisha tu kuinama, nikiinuka bahati
Mjini na jituma, kijijini...
Moyo wangu wasumbuka, yaganda ya kwangu damu
Nafsi yasononeka, hali kwani yahujumu
Mwenzenu nadhoofika, maisha yanidhulumu
Hadi lini kufinyika, tayari nishagharimu
Adimu hizi mihela, majukumu yazidia
Hamuna hata cha kula,...
Ni kweli wakati wote nakaa mwenye hasira
Ni kweli kabisa sura yangu imekunjika
Ukinitazama ni kama sina furaha yoyote
ni kama sina fani kwa lolote
Ni kweli nimesononeka
Ni kweli haya yote
Maisha yangu yote nimekuwa...
Nilipotoka ni mbali, kesho nayo majaliwa
Namshukuru Jalali, maisha kanipa mbawa
Kanilinda zote hali, kwangu tamu tu mliwa
Hapa ni kwangu manzili, mie nimebarikiwa
Raha ninayo moyoni, fikira nazo tulivu
Wa pili shajua nani,...
Ndoa jamani ndoano, mwanamwali sikimbie
Nimeshaona watano, si usemi msikie
Kuigaiga mifano, mbio mbovu mtulie
Mambo mazuri rafiki, upesi si mwendo wake
Ndoa jamani ndoano, ilo na chambo pembeni
Yavutia kwa maono, ushoboke...
Ni nyingi kelele akilini
Napotulia, akili mna kelele
Nitalia hadi lini — ninazidiwa
Napojaribu kutulia, kengele zaongezeka
Ama natokwa na wazimu mimi
Naona ni kama sijielewi
Ni nyingi kelele akilini